Main Menu

Tuesday, September 17, 2013

FBI YAMTAMBUA ALIYEUWA WATU 12 KWENYE KITUO CHA JESHI JANA

Shirika la upelelezi la Marekani, FBI, limemtambua mwanaume aliyewauwa watu 12 kwenye kituo cha jeshi la majini mjini Washington jana. 

Mtu huyo, Aaaron Alexis, mwenye umri wa miaka 34, aliwauwa watu hao kwa kuwapiga risasi, na yeye mwenyewe akauawa katika kisa hicho. FBI imesema inaamini mtu huyo aliwahi kuwa askari.
 
Awali polisi ilikuwa ikiwasaka watu wawili kwa tuhuma za mauaji hayo, lakini baadaye iling'amua kuwa mmoja wao hakuhusika. Mkuu wa polisi mjini Washington, Cathy Lanier, amesema bado hawajui sababu iliyosababisha mauaji hayo. 

Hata hivyo meya wa Washington, Vincent Gray, amesema hakuna sababu yoyote ya kuyahusisha mauaji hayo na ugaidi. Katika Ikulu ya Marekani, Rais Barack Obama amesema anaomboleza mauaji mengine ya kiholela ya kutumia bunduki.

NA dwswahili

0 comments:

Post a Comment