Main Menu

Friday, June 14, 2013

TAKUKURU MKOANI IRINGA YAKABIDHI MIPIRA KWA AJILI YA MICHUANO YA IRINGA SUPER CUP

 Mratibu wa mashindano ya Iringa super cup na mwenyekiti wa klabu ya Lipuli ya Iringa Abou Majeki akipokea msaada ya mipira kutoka kwa mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Iringa Emma Kuhanga ambao ni kati ya wadhamini wa mashindano hayo yanayofanyika mjini Iringa.
 Katibu mkuu wa chama cha soka mkoa wa Iringa ELiud Peter Mvela akipokea cheki ya milioni 14 na laki 5 kutoka kwa rais wa Lipuli madam Jesca Msavatavangu rasmi kuichukua Mkwawa stars football club zamani ikijulikana polisi Iringa.









Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa mkoani Iringa leo imekabidhi mipira miwili kwa waandaaji wa mashindano ya Iringa Super Cup yanayoshirikisha timu mbalimbali katika wilaya ya Iringa mjini.

Akikabidhi mipira hiyo ikiwa ni sehemu ya mchango wao kwa waandaji wa michuano hiyo, mkuu wa Takukuru mkoa wa Iringa Emma Kuhanga amewataka vijana kuwa mstari wa mbele kupiga vita rushwa ambayo ni adui wa haki.

Kwa upande wake mratibu wa mashindano hayo Abu Majeki amesema mipira iliyotolewa ni ishara ya michuano hiyo kuungwa mkono na wadau wa mchezo huo huku akiishukuru Takukuru kwa kuwajali vijana wa makundi yote.

0 comments:

Post a Comment