JUMLA
ya shilingi milioni 25,602,000 zimepatikana katika mechi ya Mbeya City na
Mtibwa Sugar iliyochezwa juzi katika uwanja wa kumbukumbu wa Sokoine huku timu
ya Mbeya City ikiondoka na ushindi wa goli 2-1.
Akisoma
mapato hayo Katibu wa chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA)
Selemani Harubu , alisema kati mapato hayo shilingi milioni 6,256,097 zimeenda
kwa kila timu.
Amesema,
gharama ya Vat ni shilingi milioni 3,905,388 tiketi shilingi
489,500 gharama ya mchezo 1,908,639 huku kamati ya ligi ikiondoka na
shilingi 1,908,639.
Amesema,
TFF imepata shilingi 954,818 na MREFA ikiondoka na shilingi
748,248 na uwanja ukipata shilingi 3,181,056.
Aidha,
baadhi ya mashabiki wameuomba uongozi wa MREFA kukaa meza moja ya mazungumzo
na jeshi la polisi mkoa Mbeya katika kuweka utaratibu mzuri
wa kuingia uwanjani tofauti na sasa ambapo inaelezwa kuwa baadhi ya askari
wamekuwa ndio chanzo cha vurugu.
Wamesema,
mashabiki wamekuwa wakipata usumbufu mkubwa kwa baadhi ya askari polisi ambao
hawazingatii maadili yao ya kazi kwa kuwasumbua watu hata kama hawana
kosa lolote.
Hata
hivyo katika mchezo huo mbeya city iliibuka kidedea kwa kuichabanga Mtibwa goli
2:1





0 comments:
Post a Comment