Main Menu

Monday, February 10, 2014

ASKARI MAGEREZA MKOANI MBEYA ASHIKILIWA NA POLISI KWA KUKUTWA NA TIKETI BANDIA

Kamanda wa polisi Mkoani mbeya Ndugu Ahmed Msangi akitoa ufafanunuzi juu ya tukio hilo Picha maktaba

 POLISI Mkoani Mbeya, inawashikilia watu wawili kati yao mmoja inasemekana ni askari wa  jeshi la magereza la Ruanda Koplo John Joseph kwa tuhuma za kukutwa na tiketi bandia za kuingilia uwanjani.

Akizungumzia sakata hilo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amesema tukio hilo limetokea jijini mbeya  wakati wa mpambano dhidi ya timu ya  Mbeya City na Mtibwa Sugar katika uwanja wa Sokoine uliopo Jijini Mbeya.

Amesema, askari polisi wakiwa katika harakati za kuangalia na kulinda hali ya usalama uwanjani walipata taarifa ya kwamba kuna baadhi ya watu wamekuwa na tiketi bandia.

Amefafanua kuwa askari wakishirikiana na Afisa habari wa chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Mbeya(MREFA) Lwitiko Mwandeliwa walifanikiwa kuwatia nguvuni watuhumiwa hao ambao ni Justin Alphonce(17) na John Joseph ambaye inasemekana ni askari wa jeshi la magereza na wote ni wakazi wa kota za magereza.

Amesema, tiketi hizo zilikuwa zikiuzwa kwa shilingi  3000 na kwamba watuhumiwa wote wapo rumande mpaka upelelezi utakapo kamilika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya michezo katika timu ya Mbeya City, Mussa Mapunda, amesema kitendo kilichofanywa na askari huyo si kizuri kwani viongozi wa klabu hizo wamekuwa wakitoa msaada mkubwa katika kuhakikisha timu hizo zinapiga hatua kwenye soka hasa kudhibiti mianya ya wizi wa mapato uwanjani.

0 comments:

Post a Comment