Main Menu

Sunday, July 14, 2013

MAREKANI YAINGILIA EMAIL YA RAIS WA BOLIVIA, ARGENTINA PIA YALALAMA

Rais Evo Morales wa Bolivia amesema mashirika ya kijasusi ya Marekani yamedukua email au barua pepe za viongozi wa ngazi za juu wa Bolivia.


Akizungumza Jumamosi, Morales amesema majasusi wa Marekani wameweza kusoma barua pepe za maafisa wa ngazi za juu kabisa wa Bolivia. Ameongeza kuwa ameshauriwa asitumie email na kufuatia ushauri huo amefunga akaunti yake ya barua pepe. 


Morales ameelezea wasi wasi wake kuwa yamkini Washington ikatumia taarifa ilizopata katika barua pepe hizo kupanga 'hujuma' dhidi ya nchi yake. 


Mapema wiki hii Waziri wa Mambo ya Nje wa Argentina Hector Timerman aliituhumu Marekani kuwa imedukua barua pepe za maafisa zaidi ya 100 wa serikali ya nchi hiyo. 


 Hayo yanajiri katika hali ambayo viongozi wa Bolivia, Ecuador, Venezuela na Nicaragua wametangaza kuwa tayari kumpa hifadhi Mmarekani Edward Snowden ambaye alifichua kuwa mashirika ya ujasusi ya nchi hiyo hufanya udukuzi kote duniani kwa kutumia mbinu ya kiteknolojia ya siri kuchunguza mawasiliano ya simu ya watu, barua pepe na mawasiliano mengine.

Na radio tehran swahili

0 comments:

Post a Comment