Main Menu

Thursday, March 28, 2013

MKIMBIAJI WA AFRIKA KUSINI ANAYETUHUMIWA KWA KUMUUA MPENZI WAKE PITORIUS ARUHUSIWA KUSAFIRI NJE YA SOUTH

Mahakama nchini Afrika Kusini imemruhusu Oscar Pirstorius kusafiri nje ya nchi, na hivyo kumlegezea masharti makali ya dhamana, baada ya kushtakiwa kwa mauaji ya mpenzi wake. Pistorius alikata rifaa dhidi ya mlolongo wa masharti ya dhamana ambayo alisema hayakuwa ya haki na wala hayakutakiwa. 

Jaji Bert Bam wa mahakama ya juu ya mjini Pretoria amesema uamuzi wa awali wa hakimu kumuamrisha Pistorius kukabidhi hati yake ya kusafiria haukuwa sahihi.

Hata hivyo, Pistorius atalaazimika kuwasilisha mpango wake wa safari kwa upande wa mashtaka angalau wiki moja kabla ya kusafiri, na kukabidhi tena hati yake ndani ya masaa 24 baada ya kurejea kutoka safarini. Pistorius hakuwepo mahakamani wakati uamuzi huo unatolewa.

0 comments:

Post a Comment