Main Menu

Wednesday, June 3, 2015

SEPP BLATTER HALI TETE AANZA KUCHUNGUZWA



Blatter made the announcement at a hastily organised press conference this afternoon, saying he had made the decision after considering what was best for footballSakata la kujiuzulu kwa Rais wa FIFA Joseph ‘Sepp’Blatter limechukua sura mpya Kufuatia vyombo mbalimbali vya dola kuanza kazi ya kumchunguza Rais huyo anayehusishwa na ubadhilifu wa fedha za FIFA au rushwa.

Tayari shirika la ujasusi la Marekani FBI na baadhi ya waendesha mashtaka wa nchi hiyo wameanza kumchunguza Blatter kuona kama ana hatia na kashfa za rushwa za FIFA.

Mmoja kati ya watu wa karibu wa Blatter Walter Gagg anasema kuwa “Blatter alikuwa katika hali ya kawaida sana kwa siku ya jumatatu lakini hali yake ilibadilika siku ya jana(Jumanne) kutokana na ripoti za vyombo vya Habari kuhusu kuhusika kwake na rushwa.”

Wakati hayo yakiendelea,wachunguzi wa mambo wanasema kuwa ripoti ya kurasa arobaini ya ushahidi wa mmoja kati ya wajumbe wa zamani kamati ya utendaji ya  FIFA ‘Chuck Blazer’ inaweza kuibua mambo mengi kuhusu Shrikisho hilo.

Kitendawili kikubwa ni ani atakuwa mrithi wa Blatter kati ya Michel Platini, Prince Ali Bin Hussein, David Gill, Luis Figo na Michael Van Praag.

0 comments:

Post a Comment