Main Menu

Thursday, June 4, 2015

FIGO AONDOLEWA KATIKA KIKOSI CHA MAGWIJI WA BARCELONA



Figo (in action against Chelsea) was a key part of the Barcelona team before he left for Real MadridMiongoni mwa nyota waliowahi kuitikisa dunia katika anga za kimichezo ni Luis Figo.

Kuelekea katika mchezo  wa fainali wa Ligi ya Mabingwa kati ya Juventus dhidi ya Barcelona,mchezaji nyota wa dunia Luis Figo ameondolewa katika kikosi kitakachojumuisha wachezaji waliowahi kuvichezea vilabu vya  Barcelona na Juventus.

Luis Figo amewahi kuichezea Barcelona kwa miaka mitano kabla ya kuhamia klabu ya Real Madrid.

Kitendo cha kuhamia klabu ya Real Madrid kiliwachukiza sana viongozi na mashabiki wa Barcelona kwa kumuita msaliti.

Shirikisho la soka barani Ulaya UEFA limeunda vikosi viwili vya Barcelona na Juventus dhidi ya kikosi cha dunia katika mchezo wa hisani .

Kikosi cha kwanza cha UEFA kimemjumuisha Luis Figo lakini akapingwa vikali na viongozi wa Barcelona kuwepo katika kikosi hicho.

Mjumuisho wa kikosi cha Barcelona na Juventus kitakachocheza na mastaa wengine wa dunia hiki hapa:

JUVENTUS NA BARCELONA MAGWIJI: Edwin van der Sar, Ciro Ferrara, Ludovic Giuly, Alessandro Del Piero, Giovanni van Bronckhorst, Edmílson, Fabio Cannavaro, David Trezeguet, Mark van Bommel, Gianluca Zambrotta, Deco, Eric Abidal, Christian Vieri.

KIKOSI CHA DUNIA: Jens Lehmann, Cafu, Youri Djorkaeff, Robert Pires, Predrag Mijatović, Giovane Elber, Clarence Seedorf, Rai, Christian Karembeu, Steve McManaman, Pierre van Hooijdonk, Marco Materazzi.

0 comments:

Post a Comment