Main Menu

Friday, August 1, 2014

CLINIC YA MAKOCHA 30 KUTOKA KWA WAKUFUNZI WA FC BARCELONA YAANZA LEO

IMG_6504 bacelona
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Juliana Yassoda (Katikati) akiongea na Wanahabari  kuhusu  makocha wa Timu ya Barcelona  kutoka nchini Hispania  ambao wako nchini kwa ajili ya  mafunzo ya makocha yatakayofanyika kwa muda wa siku mbili, wa kwanza kulia ni Balozi wa Spain nchini Mh. Luis Manuel Ceuesta Civis.
IMG_6513 bacelona
Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes (katikati)   kutoka timu ya Barcelona ya nchini Hispania (katikati) akitoa maelezo kwa wanahabari (hawapo pichani) kuhusu mafunzo ya siku mbili watakayotoa kwa makocha 30 wakizalendo, kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bi. Juliana Yassoda na wa kwanza kushoto ni  Kocha Daniel Bigas Alsina.
IMG_6380 bacelona
Balozi wa Hispania nchini Tanzania Mh.  Luis Manuel  Ceuesta Civis  (Kulia) akiongea na Makocha kutoka Timu ya Barcelona ya nchini Hispania katika mkutano wa Wanahabari uliofanyika jijini Dar es Salaam jana (leo), makocha hao wapo nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo ya siku mbili kwa makocha wazalendo, wa kwanza kushoto ni Kocha Daniel Bigas Alsina  na katikati ni Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes.
IMG_6530 bacelona
Makocha wa Kizalendo 30 ambao wanatarajiwa kupewa mafunzo ya siku mbili kutoka kwa makocha wa Barcelona wakiwa katika picha ya pamoja..

0 comments:

Post a Comment