Main Menu

Tuesday, October 1, 2013

WABUNGE NCHINI KENYA KUANZA UCHUNGUZI WA SHAMBULIO LA WESTGATE

Wabunge wa Kenya wamesema kuwa, kuanzia leo Jumanne wataanza uchunguzi kuhusiana na shambulio lililofanyika Septemba 21 dhidi ya kituo cha biashara cha Westgate jijini Nairobi na kusababisha makumi ya watu kuuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa. 

Asman Kamama, Mkuu wa Kamati ya Usalama wa Taifa ya Bunge la Kenya amesema kuwa kamati  za usalama wa taifa, mahusiano ya kigeni na ulinzi zitaanza kuketi kwa pamoja na kuchunguza tukio hilo kwa kina zoezi litakalochukua kwa akali masaa themanini hadi kukamilika. 


Kamama amewataka wananchi kujitokeza mbele ya kamati hizo ili kutoa ushahidi walionao ambao utaweza kusaidia  uchunguzi wao kwa maslahi ya taifa la Kenya. 

Amesema kuwa, uchunguzi huo unafanyika ili kubaini kama viongozi waliopewa jukumu la kulinda usalama wa taifa la Kenya walitekeleza majukumu yao au la. 

Shambulio hilo la kigaidi lililodumu kwa takribani siku nne lilihusisha kundi la al Shabab la nchini Somalia.

NA radio tehran

0 comments:

Post a Comment