Main Menu

Monday, September 16, 2013

TIB YAZINDUA OFISI NA TAWI KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI MJINI MBEYA


 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro (kulika) akikata utepe kuzindua ofisi za Makao Makuu ya Benki ya Maendelea Tanzania (TIB) ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na Tawi la benki hiyo Mkoa wa Mbeya iliyofanyika jijini Mbeya jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mwendeshaji wa TIB, Peter Noni na Mwenyekiti wa Bodi ya TIB, Prof. William Lyakurwa.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo Tanzania (TIB), Prof. William Lyakurwa (kushoto), akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa ofisi za Makao Makuu ya TIB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na Tawi la benki hiyo Mkoa wa Mbeya iliyofanyika jijini Mbeya. Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro na Mkurugenzi Mwezeshaji wa TIB, Peter Noni.
 Mcheza ngoma akionyesha manjonjo yake kuwaburudisha watu waliohudhuria uzinduzi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro (katikati) akiagana na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya Maendeleo Tanzania (TIB), Peter Noni (kulia), baada ya hafla ya ufunguzi wa ofisi za Makao Makuu ya TIB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na Tawi la benki hiyo Mkoani  Mbeya. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya TIB, Prof. William Lyakurwa.


0 comments:

Post a Comment