Main Menu

Wednesday, August 12, 2015

TFF, VODACOM ZAFUNGA NDOA NYINGINE YA MIAKA MINNE



Mkataba mpya

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF) limesaini mkataba mpya wa miaka mitatu (3) wa udhamini wa Ligi Kuu Tanzania bara (VPL) wenye thamani ya shilingi bilioni sita (tsh bilioni 6.6) na kampuni ya simu ya Vodacom, halfa hiyo imefanyika leo katika ofisi za makao makuu ya kampuni hiyo eneo la Mlimani City jijini Dar es salaam.

Akiongea wakati wa kusaini mktaba huo mpya, Mkurugenzi wa masoko wa kampuni ya simu ya Vodacom Kelvin Twissa, amesema kampuni yao inafurahia kuendelea kuwa sehemu ya udhamini ya ligi kuu nchini, mafanikio ya timu bora na kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa inatokana na kuwa na ligi bora ambayo inadhaminiwa na Vodacom.

Naye Rais wa TFF, Jamal Malinzi amewashukuru kampuni ya Vodacom kwa kukubali kuendelea kuidhamini ligi kuu kwa kipindi kingine cha miaka mitatu (3) na kuongeza sehemuya udhamini wao kwa asilimia 40%.

Tunaishukuru kampuni ya Vodacom kwa kuendelea kuwa sehemu ya mafanikio ya mpira wa miguu nchini, udhamini wanaotupatia unavisaidia vilabu kujiandaa na kujiendesha na mikikimikiki ya ligi na kuifanya ligi kuwa na ushindani wa hali ya juu, msimu huu ligi itakua na timu 16 tunatarajia kuendelea kushuhudia uhondo huo chini ya udhamini wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.

Mkataba huo mpya wa udhamini kwa kipindi cha miaka mitatu, umeboreshwa na kuwa na ongezeko la asilimia 40% kutoka katika mkataba wa awali uliomalizika.

Ligi Kuu ya Vodacom inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 12, 2015.


0 comments:

Post a Comment