Shirikisho
la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF) limesaini mkataba mpya wa miaka mitatu
(3) wa udhamini wa Ligi Kuu Tanzania bara (VPL) wenye thamani ya shilingi bilioni
sita (tsh bilioni 6.6) na kampuni ya simu ya Vodacom, halfa hiyo imefanyika leo
katika ofisi za makao makuu ya kampuni hiyo eneo la Mlimani City jijini Dar es
salaam.
Akiongea wakati wa kusaini mktaba huo mpya, Mkurugenzi wa
masoko wa kampuni ya simu ya Vodacom Kelvin Twissa, amesema kampuni yao
inafurahia kuendelea kuwa sehemu ya udhamini ya ligi kuu nchini, mafanikio ya
timu bora na kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa inatokana na kuwa na
ligi bora ambayo inadhaminiwa na Vodacom.
Naye Rais wa TFF, Jamal Malinzi amewashukuru kampuni ya
Vodacom kwa kukubali kuendelea kuidhamini ligi kuu kwa kipindi kingine cha
miaka mitatu (3) na kuongeza sehemuya udhamini wao kwa asilimia 40%.
Tunaishukuru kampuni ya Vodacom kwa kuendelea kuwa sehemu
ya mafanikio ya mpira wa miguu nchini, udhamini wanaotupatia unavisaidia vilabu
kujiandaa na kujiendesha na mikikimikiki ya ligi na kuifanya ligi kuwa na
ushindani wa hali ya juu, msimu huu ligi itakua na timu 16 tunatarajia
kuendelea kushuhudia uhondo huo chini ya udhamini wa kampuni ya simu za mkononi
ya Vodacom.
Mkataba huo mpya wa udhamini kwa kipindi cha miaka
mitatu, umeboreshwa na kuwa na ongezeko la asilimia 40% kutoka katika mkataba
wa awali uliomalizika.
Ligi Kuu ya Vodacom inatarajiwa kuanza kutimua vumbi
Septemba 12, 2015.
0 comments:
Post a Comment