Main Menu

Thursday, June 4, 2015

FAINAL YA KWANZA YA NBA KUPIGWA ALFAJIRI YA KESHO



Curry will keep things normal ahead of the game on Wednesday and will spend time sitting by the poolFainali ya kwanza Ligi ya mpira wa kikapu ya nchini Marekani inategemewa kufanyika alfajiri ya kesho kwa mchezo mkali na wa kusisimua kati ya Cleveland Cavaliers na Golden State Warriors.

Cleveland Cavaliers ni mabingwa wa kanda ya mashariki mara baada ya kuwatoa Atlanta Hawks huku Golden State Warriors wakiwa mabingwa wa kanda ya magharibi baada ya kuwatoa Houston Rockets.

Cleveland Cavaliers hajawahi kushinda taji la NBA ingawa wameshawahi kufika fainali za NBA mwaka 2007 pale Lebron James na wenzake walipoiongoza Cavaliers kucheza fainali.

Katika mchezo huo wa fainali Cavaliers  wakafungwa  na timu ya San Antonio Spurs.

Jiji la Cleveland halijawahai kushinda taji lolote kwa takribani miaka 51, Cleveland kama kawaida itakuwa na nyota wake katika mchezo wa fainali kama Lebron James, Kyle Irving, Kevin Love, Matt Delavedova na J.R Smith.

Kwa upande wa Golden State Warriors walichukua ubingwa wa NBA mwaka 1975 na ni miaka 40 imepita tangu wachukue ubingwa huo wa NBA.

Timu hii inajivunia uwepo wa wachezaji wake ambao wamecheza pamoja muda mrefu katika timu hiyo tangu mwaka 2009.

Wachezaji hao ni Stephen Curry, Klay Thompson, Harrison Barnes  na Draymond Green.

0 comments:

Post a Comment