Main Menu

Thursday, March 19, 2015

MAN CITY YAITIMISHA SAFARI YA TIMU ZA ENGLAND LIGI YA MABINGWA

Klabu ya Manchester city jana imehitimisha safari ya vilabu vya England katika michuano ya klabu bingwa barani Ulaya baada ya kutupwa nje na klabu ya Barcelona kwa jumla ya mabao matatu kwa moja.

Katika mchezo wa jana Man city ilikubali kipigo cha bao moja kwa bila katika dimba la Nou camp kwa goli la kiungo Rakitic na kufanikiwa kutinga robo fainal.

Mshambuliaji wa Man city Kun Aguero alikosa penalt katika mchezo huo na hivyo kufanya matokeo ya jumla Barca kushinda kwa 3-1.

Timu zote nne za England zilizoshiriki michuano hiyo zimetupwa nje, tatu kati yao kwenye mzunguko wa pili na moja ambayo ni liverpool kwenye hatua ya makundi.

Timu zilizotolewa katika hatua ya mtoano ni Chelsea, Arsenal na Manchester city.

Manchester City were eliminated at the last 16 stage after failing to overturn their first-leg deficit against Barcelona
Sergio Aguero baada ya kukosa penalt iliyodakwa na kipa wa barca.
Manchester City's players leave the Nou Camp looking glum after being eliminated from the Champions League
Wachezaji wa Manchester City wakitoka Nou camp vichwa chini.
Messi taunts Martin Demichelis and the Man City defence on the edge of the penalty area during a classy performance from the Argentine
Messi akikabwa na Martin Demichelis pamoja na wachezaji wengine wa Man City katika eneo la hatari
Messi receives a hug from Martin Demichelis and David Silva after the final whistle at the Nou Camp
Haikua na jinsi mwisho wa siku ilibidi wampongeze raia huyu wa argentina Messi kwa mpira mkubwa alioupiga, wanaompongeza ni Martin Demichelis na David Silva.

0 comments:

Post a Comment