Main Menu

Friday, August 23, 2013

RAIS RAJOELINA AAFIKI KUTOSHIRIKI URAIS MADAGASCAR

Rais wa serikali ya mpito ya Madagascar amekubali kuondolewa jina lake miongoni mwa majina ya viongozi wasiostahiki kuwa wagombea wa kiti cha urais nchini humo. 


Rais Andry Rajoelina wa serikali ya mpito ya Madagascar jana alikubali rasmi kuondolewa jina lake miongoni mwa wagombea wanaofaa kushiriki katika uchaguzi ujao wa rais nchini humo.


Amesisitiza kuwa atakabidhi madaraka kwa njia ya kidemokrasia kwa rais atakayechaguliwa nchini humo baada ya kufanyika uchaguzi. 


Hii ni katika hali ambayo Lalao Ravalomanana mke wa Rais wa zamani wa Madagascar amepinga uamuzi wa mahakama maalumu ya uchaguzi ya kuliondowa jina lake katika orodha ya wagombea wa kiti cha urais .

NA radio tehran

0 comments:

Post a Comment