TIMU YA TAIFA YA TAHITI YAAMBULIA MAGOLI 24 KWENYE MICHEZO 3 KATIKA KOMBE LA MABARA NCHINI BRAZIL
 
Katika hatua ya mwisho ya michuano ya 
makundi  kwenye mashindano ya kombe la 
mabara la Confederations Cup nchini Brazil 
mabingwa wa dunia Uhispania 
waliwaonyesha mabingwa wa Afrika, Nigeria 
kandanda ya pasi fupi na kuwachapa mabao 
matatu kwa bila.
Katika mechi nyingine Uruguay haikuwa na 
huruma  na Timu ya Tahiti ya wachezaji wa 
ridhaa karibu  wote. 
Kwa mara nyingine Tahiti iligeuzwa kapu la 
magoli kwa kuchabangwa mabao manane 
kwa bila.
Uhispania na Uruguay zimeingia katika nusu 
fainali, ambapo Uhispania itapambana na 
Italia na Uruguay itamenyana na Brazil.
 
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment