Main Menu

Tuesday, July 21, 2015

KLABU YA MBEYA CITY YATANGAZA ZABUNI YAA UAGIZAJI NA UUZAJI WA VIFAA VYA KLUBU HIYO.



Mbeya City Council F.C inakaribisha kampuni zenye uwezo wa kufanya kazi na club yetu.

Kazi zinazotangazwa ni kama ifutazo:
I.    Kuwa mwagizaji wa vifaa mbalimbali vya club
II.    Kuuza vifaa mbalimbali vya club
Zabuni hii inafuati utekelezaji wa club kutaka kukuza mapato yake ili iweze kujijenga msingi imala ya mapato na hivyo kuiwezesha kuendesha shughuli zake mbalimbali.

Mwombaji anatakiwa atimize masharti yafuatayo.
1. Awe na Leseni hai ya biashara husika
2. Awe amesajiliwa kama mlipa kodi
3. Maelezo ya kampuni yaani Company profile ikieleza aina ya kampuni au biashara unayoifanya na eneo ilipo.

4. Waombaji wawe ni makampuni yaliyosajiliwa kisheria na waambatanishe vivuli vya nyaraka zinazoonyesha uhalali wa uwepo wa mwombaji. Pia muombaji aonyeshe anwani ya ofisi yake (physical address).

5.Bahasha zenye zabuni zifungwe na lakiri zikionyesha jina na namba ya zabuni inayoombwa zikielekezwa kwa anuni ya Katibu Mkuu Mbeya City Council
F.C, S.L.P 149, Mbeya na ziwasilishwe ofisi ya Timu iliyopo Ukumbi wa
Mkapa.
        Kwa maelezo wasiliana na;
        Katibu Mkuu
        Mbeya City  Council F.C
        S.L.P 149,Mbeya.
          Simu  N0: 0718732626

6.Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 03.08.2015 saa 4.00 asubuhi.

Katibu Mkuuu
Mbeya City Council F.C

0 comments:

Post a Comment