Kocha wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho
amesema kuwa wachezaji Felipe Luis na Mohamed Salaha wanaruhusiwa kondoka
katika klabu hiyo endapo watapewa ofa nzuri toka kwa timu zinazowahitaji.
Felipe Luis amejiunga na klabu ya Chelsea
kitokea klabu ya Atletico Madrid kwa kiasi cha pauni milioni 15.8 .
Felipe Luis amekosa nafasi katika kikosi cha
kwanza cha Chelsea mbele ya beki Cesar
Azpiliqueta ambaye amekuwa akitumiwa sana na kocha Jose Mourinho kama beki wa
kushoto.
Kwa upande wa Mohamed Salah,alikuwa kwa mkopo
katika klabu ya Fiorentina lakini amekosa namba katika kikosi cha kwanza cha
Chelsea.
0 comments:
Post a Comment