Main Menu

Thursday, June 4, 2015

STARS ILE ILE KUONDOKA LEO KUJIANDAA KUIVAA MISRI, NOOIJ AAHIDI USHINDI



Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Mart Nooij ametangaza kikosi cha wachezaji 23 watakaoondoka leo jioni kuelekea Addis Ababa nchini Ethiopia kuweka kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Misri

Mart Nooij amesema watatumia kambi ya Ethiopia kujiandaa na mchezo wa Misri, vijana wapo katika hali nzuri na wameahidi kupambana kuhakikisha wanafanya vizuri katika mchezo huo.

Mchezo kati ya Misri na Tanzania unatarajiwa kuchezwa Juni 14, katika uwanja wa Borg El Arab jijini Alexandria, ikiwa ni mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa Afrika (AFCON) mwaka  2017.

Kikosi cha Stars kinaondoka saa 11 jioni kwa Shirika la ndege la Ethiopia ambapo inatarajiwa kuwasili jiji la Addis Ababa majira ya saa 1 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Wachezaji wanaosafiri kuelekea nchini Ethiopia ni  Deogratias Munish, Aishi Manula, Mwadini Ali, walinzi Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Erasto Nyoni, Nadir Haroub, Aggrey Morris, Mwinyi Haji, Salum Mbonde na Juma Abdul.

Wengine ni Mwinyi Kazimoto, Abdi Banda, Salum Telela, Frank Domayo, Jonas Mkude, Said Ndemla, washambuliaji Saimon Msuva, John Bocco, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samatta,Mrisho Ngasa na Juma Liuzio.

Msafara wa Taifa Stars utaongozwa na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Vedastus Lufano na Geofrey Irick Nyange “Kaburu”.

0 comments:

Post a Comment