Main Menu

Sunday, June 7, 2015

BAADA YA KUKOSA UBINGWA WA UEFA, BUFFON KUENDELEA KUDAKA HADI MIAKA 40



The legendary Italian stopper waves to the crowd at the final whistle as he reflects on a disappointing defeat Baada ya kupoteza mchezo wa fainali dhidi ya Barcelona hapo jana, kipa wa klabu ya Juventus na timu ya taifa ya Italia Gianluigi ‘Gigi’ Buffon amesema kuwa ataendelea kudaka mpaka atakapofikisha umri wa miaka 40.

Kwa sasa Buffon ana miaka 37 na bado anaamini ana nguvu za kuweza kudaka kwa miaka mitatu ijayo.

Endapo Buffon atadaka mpaka umri wa miaka 40, atafikia rekodi ya makipa wengine ambao walifikisha umri huo huku wakidakia vilabu vyao na timu ya taifa ya Italia.

Makipa hao ni pamoja na Dino Zoff aliyedakia Italia katika fainali za kombe la dunia la mwaka 1982 akiwa na umri wa miaka 40.
 The Italian goalkeeper kept his side in the final with two saves he made early in either half of the showpiece 
Mbali na Dino zoff, kipa mwingine aliyeweka rekodi ya kudaka akiwa na umri mkubwa nchini Italia ni Walter Zenga.

Zenga alidakia Inter Milan akiwa na umri wa miaka 39.

Historia inatuonesha kuwa wapo makipa wengi waliowahi kudaka wakiwa na umri mkubwa katika medani ya soka.

Makipa hao ni pamoja na Brad Fridel wa Marekani amedaka mpaka akiwa na umri wa miaka 44, Edwin Van Der Sar aliidakia manchester United mpaka akiwa na umri wa miaka 38.Gianluigi Buffon reacts after Neymar (not pictured) scored Barcelona's second goal of the evening in Berlin 

0 comments:

Post a Comment