Main Menu

Sunday, June 7, 2015

FAINAL YA PILI YA NBA KUPIGWA ALFAJIRI YA KESHO



Stephen Curry (No 30, with ball) of Golden State leaps to shoot against Timofey Mozgov of Cleveland in Game One of the NBA finalsFainali ya pili ya Ligi ya mpira wa kikapu ya NBA itaendelea tena alfajiri ya kesho kwa kuzikutanisha timu ya Golden State Warriors na Cleveland Cavaliers.

Katika mchezo wa kwanza timu ya Golden State Warriors ilipata ushindi wa pointi 108 dhidi ya 100 za Cleveland Cavaliers.

Katika mchezo wa kwanza, Cleveland walimpoteza mchezaji wao Kyle Irving  aliyeumia kifundo cha mguu na kufanyiwa operesheni ya kifundo hicho huku Kevin Love akiumia bega.

Katika mchezo wa kwanza Lebron James alifunga pointi 44 peke yake na anategemewa sana kufanya vizuri katika mchezo wa leo.

Kwa upande wa Golden State Warriors wenyewe wataendelea kuwa na wachezaji wake wote nyota ambao ni Stephen Curry, Klay Thompson na Draymond Green.

0 comments:

Post a Comment