Bi. Shida Mapele akiwa hospitalini kupatiwa matibabu baada ya kujeruhiwa vibaya na mchumba wake.
Na Abdulaziz Video
Huku Dunia ikiwa Imeazimisha Siku 16 za harakati dhidi
ya ukatili wa kijinsia kwa wanawake,huko Wilayani Liwale Mkoani
Lindi, Mkazi Mmoja wa kijiji cha Naluleo aliefahamika kwa Jina la
Shida Mapele amejeruhiwa vibaya kwa Mapanga na Mchumba wake na kumsababishia
ulemavu wa kudumu baada ya kumkata mkono wa kulia na kumjeruhi
katika baadhi ya viungo vyake.
Hii ni ishara ya kuhusisha ukatili dhidi ya wanawake na haki za
binadamu na uvunjaji wa haki za binadamu licha ya Mtuhumiwa
kufikishwa mbele ya Sheria,Wanawake wilayani Humo wametakiwa kutetea
haki zao huku wakiomba sheria ichukue mkondo wake dhidi ya ukatili huo
uliofanywa na Bw. Ally Burian ambae anashiliwa na Jeshi la Polisi.
Akiongea na Ripota wa Globu ya Jamii Wilayani humo,Mratibu wa Asasi ya kutetea
wanawake na watoto(Liwopac)Bi Hidaya Chikawe alieleza kuwa licha ya
harakati zinazofanywa na wanawake kuelimisha jamii Bado Vitendo hivyo
vinashika kasi wilayani humo.
“Hakika kwa tukio hili ni Ishara tosha inayodhihirisha kuwepo kwa
ukatili wilayani humu,Hapo Awali tulizoea kusikia katika mikoa ya
wenzetu lakini sasa Dunia imebadilika tunashuhudia matukio haya mara
kwa mara”alieleza Chikawe.
Aidha aliwataka akina mama wa liwale kuanza kujitetea kwa kufichua
uhalifu unaojitokeza kutokana na Takwimu ya mwaka jana inaonyesha
matukio hayo kuwepo kwa 2% lakini sasa hali inaongezeka kila mara
hususan kipindi hiki cha mauzo ya korosho.
Kwa Upande wao baadhi ya akinamama walisema licha ya historia ya
matukio mabaya kutokea wilayani humo tukio hili la kumsababishia
ulemavu mwanamke huyo kutokana na kukatwa kwa mapanga.
Walieleza walivyoguswa na tukio hilo huku wakitoa wito kwa jamii na serikali
kuchukua hatua kali kwa wahusika wanaobanika na kukamatwa.
Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wamekuwa katika
mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia ambapo hivi karibu Mwenyekiti
wa Mtandao wa Polisi wanawake mkoa wa Lindi,Kamishna msaidizi wa
Polisi Bi Renatha Mzinga alianzisha kampeni ya kutoa elimu kwa jamii
kuhusiana na matukio hayo katika maadhimisho ya siku 16 za ukatili
dhidi ya Mwanamke ambapo walifanikisha kutoa misaada na usafi katika
kambi ya wazee na walemavu
0 comments:
Post a Comment