UHAI CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI NOV 17
Michuano
 ya Kombe la Uhai inayoshirikisha wachezaji wenye umri chini ya miaka 20
 wa klabu za Ligi Kuu inaanza kutimua vumbi Novemba 17 mwaka huu katika 
viwanja vya Karume na Azam Complex, Dar es Salaam.
Droo
 ya michuano hiyo inayodhaminiwa na Maji Uhai imefanyika leo (Novemba 8 
mwaka huu) mbele ya waandishi wa habari katika ofisi za Shirikisho la 
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambapo timu zimepangwa katika makundi 
matatu.
Kundi
 A linaundwa na timu za Azam, Coastal Union, JKT Ruvu Stars, Mbeya City 
na Yanga, wakati kundi B ni Ashanti United, Mgambo Shooting, Oljoro JKT 
na Ruvu Shooting. Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, Rhino Rangers na Tanzania 
Prisons ndizo zinazounda kundi C.
Mechi
 za ufunguzi kundi A Novemba 17 mwaka huu ni kati ya Azam na Coastal 
Union (saa 2 asubuhi- Karume), Yanga na Mbeya City (saa 8 mchana- 
Karume). Kundi B ni Ruvu Shooting na Ashanti United (saa 4 asubuhi- 
Karume), Oljoro JKT na Simba (saa 10 jioni- Karume).
Kagera
 Sugar na Mtibwa Sugar (saa 2 asubuhi- Azam) na Rhino Rangers na 
Tanzania Prisons (saa 10 jioni- Azam) ndizo zitakazocheza mechi za 
ufunguzi Novemba 17 mwaka huu katika kundi C.
Robo
 fainali ya michuano hiyo itachezwa Novemba 24 na 25 mwaka huu wakati 
nusu fainali itapigwa Novemba 26 na 27 mwaka huu. Mechi ya kutafuta 
mshindi wa tatu na ile ya fainali zitachezwa Novemba 30 mwaka.
TANZANITE YATUA SALAMA MAPUTO
Kikosi
 cha timu ya Taifa ya wanawake chini ya miaka 20 (Tanzanite) kimewasili 
salama jijini Maputo, Msumbiji tayari kwa mechi ya marudiano ya raundi 
ya kwanza ya Kombe la Dunia itakayochezwa kesho (Novemba 9 mwaka huu).
Kwa
 mujibu wa kiongozi wa msafara wa Tanzanite, Kidao Wilfred ambaye pia ni
 mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania 
(TFF), timu hiyo chini ya Kocha wake Rogasian Kaijage ilifanya mazoezi 
yake ya kwanza jana asubuhi.
Tanzanite
 itafanya mazoezi yake ya mwisho leo (Novemba 8 mwaka huu) kwenye Uwanja
 wa Taifa wa Zimpeto ambao ndiyo utakaotumika kwa mechi hiyo 
itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni kwa saa za Msumbiji.
Nao
 wachezaji waliobaki kumalizia mtihani yao ya kidato cha nne wameondoka 
leo saa 11 jioni kwa ndege ya LAM wakiongozwa na naibu kiongozi wa 
msafara, Khadija Abdallah Nuhu ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya
 Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA). 
KESSY KUSIMAMIA MECHI YA KOMBE LA DUNIA
Shirikisho
 la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua Lina Kessy kuwa kamishna wa 
mechi ya Kombe la Dunia Kanda ya Afrika kwa wanawake chini ya umri wa 
miaka 20 kati ya Afrika Kusini na Botswana.
Mechi
 hiyo ya marudiano ya raundi ya kwanza itachezwa nchini Afrika Kusini, 
Novemba 9 mwaka huu. Waamuzi kutoka Zambia ndiyo watakaochezesha mechi 
hiyo namba kumi.
Waamuzi
 hao wataongozwa na Glads lengwe atakayepuliza filimbi wakati mwamuzi 
msaidizi namba moja ni Bernadette Kwimbira kutoka Malawi, namba mbili ni
 Mercy Zulu na mezani atakuwepo Sarah Ramadhani, wote wa Zambia. 
Afrika
 Kusini ilishinda mechi ya kwanza ugenini mabao 5-2. Mshindi wa mechi 
hiyo atacheza raundi ya pili na mshindi wa mechi kati ya Tanzania na 
Msumbiji.
MECHI YA JKT RUVU, COASTAL YAINGIZA LAKI 2/-
Mechi
 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya wenyeji JKT Ruvu na Coastal Union 
ya Tanga iliyochezwa juzi (Novemba 6 mwaka huu) Uwanja wa Azam Complex, 
Dar es Salaam imeingiza sh. 201,000.
JKT
 Ruvu iliibuka na ushindi wa bao 1-0 katika mechi hiyo namba 85 na 
kushuhudiwa na watazamaji 67 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 
3,000 na 10,000.
Kila klabu ilipata mgawo wa sh. 39,010 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 30,661.
Mgawo
 mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 19,835, tiketi sh.
 38,100, gharama za mechi sh. 11,901, Bodi ya Ligi sh. 11,901, Mfuko wa 
Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 5,950 na Chama cha Mpira wa Miguu 
Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 4,628.
Nayo
 mechi kati ya Ashanti United na Simba iliyochezwa juzi Uwanja wa Taifa 
imeingiza sh. 24,931,000 ambapo kila klabu ilipata mgawo wa sh. 
5,333,590.
Wakati
 huo huo, mechi za jana (Novemba 7 mwaka huu) kati ya Yanga na Oljoro 
imeingiza sh. 34,902,000 kutokana na watazamaji 6,045 ambapo kila klabu 
imepata sh. 7,812,477.95. Mechi ya Azam na Mbeya City iliyochezwa Azam 
Complex yenyewe imeingiza sh. 15,973,000 kwa watazamaji 4,857 na kila 
klabu imepata sh. 3,953,162.
WATATU WAOMBEWA ITC KUCHEZA UJERUMANI
Watanzania
 watatu wameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) na Chama cha 
Mpira wa Miguu Ujerumani (DFB) ili wacheze mpira wa miguu nchini humo.
Wachezaji
 hao ni Charles Mishetto na David Sondo wanaombewa hati hiyo ili waweze 
kujiunga na timu ya SpVgg 1914 Selbitz, wakati Eric Magesa ameombewa 
kibali hicho ili achezee timu ya klabu ya SC Morslingen.
Hata
 hivyo, katika maombi hayo DFB haikuleza hapa nchini walikuwa wakicheza 
katika klabu zipi. Wachezaji wote wameombewa hati hiyo kama wachezaji wa
 ridhaa.
Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)





0 comments:
Post a Comment