Main Menu

Tuesday, August 6, 2013

TAZARA MAJANGA TENA: WAFANYAKAZI WADAI MSHAHARA WA MIEZI 3, WAGOMA KWA SAA KADHAA, WATANGAZA KWENDA KWA WAZIRI MKUU


Wafanyakazi wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) leo wamefanya mgomo wa saa chache kushinikiza Menejimenti iwalipe mshahara wao wa miezi mitatu. 

 Wakizungumza wakati wa mkutano wao wa kujadili matatizo yao ikiwemo na hatma ya malipo ya mshahara wao wafanyakazi hao wamesema hawawezi tena kuendelea na kazi kwani kwa sasa wana njaa ya miezi mitatu na hivyo kuitaka Menejimenti kuwalipa kwanza mishahara yao na ndipo waendele na kazi. 
 Kwa upande wake Menejimenti imewataka wafanyakazi hao kuvumilia kwani tatizo lao linashughulikiwa. 

Hata hivyo wafanyakazi hao wameazimia kwenda kwa Waziri Mkuu  kuwasilisha suala lao.
Mmoja wa wafanyakazi wa TAZARA, Charles Sumai akiongea kwa hasira wakati wa mkutano wao huo.
Sehemu ya abiria wanaosafiri kwa treni ya TAZARA wakiwa nje ya kituo na mizigo yao baada ya safari ya reni iliyokuwa iwe saa 9.50 kuahirishwa mpaka saa 2 usiku kufuatia sakata hilo leo.
Sehemu ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) wakiwa kwenye mkutano wao kujadili matatizo mbalimbali ikiwemo hatma yao ya kutolipwa mshahara wa miezi mitatu kuanzi Mei, juni na Julai. Mkutamo huo ulifanyika kwenye ofisi za TAZARA, Dar es Salaam leo mchana.

NA michuziblog


0 comments:

Post a Comment