Main Menu

Thursday, August 8, 2013

MUGABE ASEMA MATOKEO YA UCHAGUZI NCHINI ZIMBABWE NI JIBU TOSHA KWA NCHI ZA MAGHARIBI

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amesema kuwa matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika siku chache zilizopita nchini humo na mahudhurio makubwa ya wananchi kwenye zoezi hilo ni jibu kali kwa siasa za nchi za Magharibi.


Mugabe amesema kuwa matokeo ya uchaguzi huo na jinsi wananchi walivyoshiriki kwa wingi katika zoezi hilo vimezivunja moyo nchi za Magharibi. 


Ameongeza kuwa nchi za Magharibi ni maadui wa Zimbabwe na kwamba wananchi wametoa kipigo kikali kwa siasa za nchi hizo dhidi ya Zimbabwe.


Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe, Rais Robert Mugabe alimshinda mpinzani wake mkubwa Morgan Tsvangirai wa chama cha MDC kwa kupata asilimia 61 ya kura.


Chaguzi za Rais na Bunge za Zimbabwe zilifanyika tarehe 31 mwezi uliopita wa Julai.

0 comments:

Post a Comment