Main Menu

Monday, June 17, 2013

NELSON MANDELA AENDELEA VIZURI BAADA YA KUWEPO HOSPITAL KWA SIKU TISA

Rais  wa  zamani  wa  Afrika  kusini  Nelson Mandela anasemekana  kuwa  hali  yake  inaendelea  vizuri  baada ya  kuwapo  hospitali  kwa  muda  wa  siku  tisa  sasa.

Rais Jacob Zuma  amesema  kuwa  Mandela  ameendelea kuwa  pamoja  na  familia  yake  katika  hospitali  ya  mjini Pretoria  ambako  anapatiwa  matibabu.

Katika  hotuba, Zuma  pia  alitoa  wito  wa  watu  kujiunga  nae  ili kumtakia  Mandela  siku  njema  ya  maadhimisho  ya  siku ya  kinababa. 

Mandela  mwenye  umri  wa  miaka  94 anasumbuliwa  na  maambukizi  katika  mapafu, ikiwa  ni mara  ya  nne  kulazwa  hospitalini  kwa  ajili  ya  matibabu tangu  Desemba  mwaka  jana.

0 comments:

Post a Comment