Main Menu

Monday, July 20, 2015

KHATROUM , GOR MAHIA ZATOA VIPIGO VYA PAKA MWIZI KAGAME CUP



Mabingwa mara tano wa michuano ya Kombe la Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya, leo imeshinda mchezo wake wa pili mfululizo baada ya kuichapa KMKM ya Visiwani Zanzibar kwa mabao 3-1.

Mabao ya Gor Mahia yalifungwa na mshambuliaji Meddy Kagere bao moja, Michael Olunga aliyefunga mabao 2, huku bao la kufutia machozi la KMKM likifungwa na Matheo Anthony.

Katika mchezo wa awali uliochezwa saa 8 mchana, Khartoum ya Sudan iliichapa timu ya Telecom ya Djibout kwa mabao 5- 0, mabao ya Khartoum yalifungwa na Wagdi Abdallah, Ousmaila Baba, Murwan Abdallah, na Salah Bilal aliyefunga mabao mawili.

Kwa matokeo hayo ya leo Gor Mahia wamefikisha pointi 6, wakifuatiwa na Khartoum yenye pointi tatu sawa na KMKM wakipishana kwa idadi ya magoli ya kufunga na kufungwa.

0 comments:

Post a Comment