Mabingwa mara tano wa michuano ya Kombe la Vilabu Bingwa
Afrika Mashariki na Kati timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya, leo imeshinda
mchezo wake wa pili mfululizo baada ya kuichapa KMKM ya Visiwani Zanzibar kwa
mabao 3-1.
Mabao ya Gor Mahia yalifungwa na mshambuliaji Meddy
Kagere bao moja, Michael Olunga aliyefunga mabao 2, huku bao la kufutia machozi
la KMKM likifungwa na Matheo Anthony.
Katika mchezo wa awali uliochezwa saa 8 mchana, Khartoum
ya Sudan iliichapa timu ya Telecom ya Djibout kwa mabao 5- 0, mabao ya Khartoum
yalifungwa na Wagdi Abdallah, Ousmaila Baba, Murwan Abdallah, na Salah Bilal
aliyefunga mabao mawili.
Kwa matokeo hayo ya leo Gor Mahia wamefikisha pointi 6,
wakifuatiwa na Khartoum yenye pointi tatu sawa na KMKM wakipishana kwa idadi ya
magoli ya kufunga na kufungwa.
0 comments:
Post a Comment