Main Menu

Monday, July 20, 2015

KAGAME CUP KUENDELEA KESHO KWA MICHEZO MITATU



 
Michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea kutimua vumbi jijini Dar es salaam, kesho jumanne itaingia katika siku ya nne kwa kuwakutanisha  Azam FC dhidi ya Malakia kutoka Sudani Kusini, mchezo utakochezwa katika uwanja wa Taifa majira ya saa 10 kamili jioni.

Mchezo wa kwanza utakaoanza majira ya saa 8 kamili mchana uwanja wa Taifa utazikutanisha timu za Al Shandy ya Sudan dhidi ya LLB ya Burundi, huku uwanja wa Karume majira ya saa 10 kamili jioni Heegan FC ya Somalia wataonyeshana ubavu dhidi ya APR kutoka Rwanda.

Jumatano kutakua na michezo mitatu ambapo mchezo wa kwanza uwanja wa Taifa utawakutanisha Khartoum ya Sudan dhidi ya KMKM ya Zanzibar saa 8 mchana, huku uwanja wa Karume saa 10 jioni KCCA ya Uganda watawakaribisha Adama City kutoka Ethiopia.

Katika uwanja wa Taifa jumatano saa 10 jioni, Telecom ya Djibout watakua wenyeji wa Yanga SC ambayo kocha wake mkuu Hans Van Der Pluijm ameahidi kupata ushindi katika mchezo huo.

Hans amesema mchezo wa ufunguzi dhidi ya Gor Mahia walipoteza kutokana na kucheza pungufu kwa takribani dakika 60, hivyo anawaanda vijana wake kufanya vizuri siku ya jumatano na kuwapa furaha wanachama na wapenzi wa Yanga SC.

0 comments:

Post a Comment