Main Menu

Sunday, July 19, 2015

MESSI AZINDUA UJENZI WA UWANJA GABON



Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona Lionel Messi yupo Barani Afrika katika nchi ya Gabon kuweka jiwe la msingi  la ujenzi wa uwanja mpya utakaofahamika kama  Port Gentil.

Uwanja huo utatumika katika fainali za Afcon mwaka 2017 nchini Gabon.

Ujio wa Messi nchini Gabon unatokana na mualiko aliopewa na Rais wa Gabon Ali Bongo Ondimba.

Baada ya kufika uwanja wa ndege,Messi alipokewa na maelfu ya wananchi wa Gabon waliofika kumuona mchezaji huyo.
 
Katika msafara huo Messi aliongozana pia na kiungo mshambuliaji wa zamani wa timu ya Barcelona Deco.

0 comments:

Post a Comment