Joseph Maria Bartomeu amechaguliwa tena kuwa Rais wa
Barcelona kwa kumshinda mpinzani wake Juan Laporta.
Bartomeu amepata kura kwa asilimia 54.63 kati ya kura zote
zilizopigwa na wanachama wa Bracelona katika uchaguzi wa klabu hiyo hapo jana.
Taarifa za ndani toka klabu ya Barcelona zinasema kuwa ushindi
wa Bartomeu unatokana na mafanikio ya Barcelona msimu uliopita kwa timu hiyo kuchukua
makombe matatu.
Makombe hayo ni pamoja na Ligi ya Mabingwa Ulaya ,Kombe
la mfalme nchini Hispania na kombe la Ligi Kuu ya soka nchini Hispania La Liga.
Uchaguzi huo ulihudhuliwa na wachezaji wa Barcelona
wakiongozwa na nahodha wa klabu hiyo Andres Iniesta.
0 comments:
Post a Comment