Main Menu

Wednesday, June 17, 2015

GOLDEN STATE WARRIORS MABINGWA WA NBA BAADA YA MIAKA 40



The Golden State Warriors celebrate with the NBA Championship Trophy after beating CleavlandFainali ya Ligi ya mpira wa kikapu ya NBA imefikia tamati asubuhi ya Leo Kwa mchezo wa sita kati ya Golden State Warriors dhidi ya Cleveland Cavaliers.

Katika mchezo huo, timu ya Golden State Warriors imefanikiwa kuchukua taji la NBA baada ya kuifunga timu ya Cleveland Cavaliers kwa pointi 107 kwa 95 na hivyo kushinda kwa michezo 4-2.
 Klay Thompson (left) and Stephen Curry pose with the trophy after the title was secured in Cleveland
Kwa ushindi huo Golden State Warriors imefanikiwa kuchukua taji la NBA kwa mara ya nne katika historia ya timu hiyo ambapo imewachukua miaka 40 tangu walipotwa ubingwa mara ya mwisho mwaka 1975.

Katika mchezo huo wachezaji wa Golden State Warriors Andre Iguodala na Stephen Curry walifunga pointi 25 kila mmoja huku Lebron James akifunga pointi 32 peke yake kwa upande wa Cleveland Cavaliers.
 Despite another superb display, LeBron James was not able to steer his side to victory on their home court
Mchezaji wa Warriors Andre Iguodala amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mashindano.
 Finals MVP Andre Iguodala dunks the ball during the second half as Golden State clinched the trophy

0 comments:

Post a Comment