Klabu ya Dar
es Salaam Young Africans kupitia baraza la wazee wameipa siku tano Halmashauri ya Manispaa ya
Ilala kuwapa jibu la maombi yao ya kuongezewa eneo la Jangwani kwa ajili ya
ujenzi wa Uwanja wa michezo.
Katibu wa
Baraza hilo Ibrahim Akilimali, amesema wanashangaa kuona manispaa hiyo
ikiendelea kuwapiga danadana licha ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki
kulikabidhi suala hilo kwa viongozi wa Manispaa ya Ilala.
Wazee hao
wamedai katika kikao cha manispaa hiyo kilichokaa jana walishangaa kuona viongozi
wao wanatolewa nje ya ukumbi wakati maombi yao yakijadiliwa ilihali walipewa
mualiko.
0 comments:
Post a Comment