Vituo vitatu vikubwa vya televisheni nchini Kenya vimezima mitambo yao
baada ya Mahakama Kuu nchini humo kutoa uamuzi kwamba vinapaswa kuingia
katika mfumo wa utangazaji wa dijitali na kuachana na mfumo wa analojia.
Vituo hivyo vya Standard Group, Nation Media Group na Royal Media
Services, awali vilikwenda mahakamani kuomba kuahirishwa muda wa kuhamia
kwenye mfumo huo, hadi masuala kadhaa yatakapofafanuliwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment