Main Menu

Sunday, June 16, 2013

MAREKANI KUMLINDA RAIS WAO WENYEWE, MELI MAALUM YA KIVITA KUTIA NANGA DAR.

Idara ya Ujasusi ya Marekani imeweka bayana kwamba inajitegemea kwa ulinzi katika ziara nzima ya Rais Barack Obama kwa nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania, Afrika Kusini na Senegal.
Kwa mujibu wa taarifa ya idara hiyo, katika kuhakikisha usalama wa kutosha wakati wa ziara ya Obama tayari maofisa wao wameshakamilisha maandalizi ya kiusalama katika nchi zote anazotarajiwa kutembelea.
Meli ya kivita kutua bandarini
Katika kuchukua hatua hizo, meli kubwa kabisa ya kivita yenye hospitali maalum zipo tayari kwa ya kambi maalumu katika bandari maalum za nchi atakazotembelea, kwa ajili ya kukabiliana na dharura yoyote ya kiafya ya Obama na familia yake.
Ili kuwawezesha maofisa wa kijasusi wa Marekani, ndege ya kijeshi ndiyo itakayobeba magari 56 zikiwemo limousine 14 na magari matatu maalumu ya kubeba mizigo.
Malori hayo yatakuwa yakibeba vioo ambavyo ni vizuizi maalumu vya risasi na milipuko kwa ajili ya kuongeza ulinzi kwenye hoteli atakazolala yeye na familia yake.
Ndege za kivita kutawala anga
Ndege za kivita zitakuwa zikiruka kwa zamu wakati wote muda wa sasa 24 kwa ajili ya kuhakikisha ulinzi katika sehemu atakayokuwa Rais Obama na kudhibiti anga yote kwa wakati huo dhidi ya ndege yoyote ngeni itakatosogea usawa wao.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Mwananchi, hakuna Maandalizi ya safari hiyo ambayo tayari yamekamilika yanapolinganishwa na safari nyingine za aina hiyo zilizowahi kufanyika, waraka maalumu kuhusu suala la usalama unaonesha kwamba kumekuwa na juhudi za ziada zakuhakikisha ulinzi wa Amiri jeshi huyo Mkuu wa Marekani akiwa nje ya nchi.
Kabla ya safari yake kwa nchi za Afrika, Obama atatembelea Ireland na Ujerumani ikiwa ni sehemu ya kuongeza changamoto inayokabili masuala ya usalama wake.
Lakini zaidi, safari ya Obama kwa nchi za Afrika inadhaniwa kuwa inayolazimisha waandaaji kuwa na umakini wa hali ya juu na kuifanya iwe aghali zaidi katika utawala wa Obama kuliko ziara katika nchi za ulaya, kwa mujibu wa wataalamu wa mipango.


Familia ya rais huyo inatarajiwa kutembelea nchi tatu za Afrika, ikiwemo Tanzania, Afrika Kusini na Senagal kuanzia Juni 26 hadi Julai 3 mwaka huu.
Serikali ya Marekani inahakikisha kwamba inasimamia kwa silimia 100 ulinzi wa familia hiyo inapokuwa nje ya nchi na haihitaji kutumia vyombo vya usalama vya nchi husika ikiwemo polisi, majeshi, na huduma za hospitali.
Safari yaahirishwa
Katika ziara ya Obama nchini Tanzania, safari ya kutembelea Mbuga ya Wanyama ya Mikumi yeye pamoja na familia yake imeahirishwa ili kupunguza ukubwa wa gharama katika safari yake.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi, Obama hatatembelea tena mbuga za wanyama kama ilivyopangwa awali, bali imependekezwa kwamba sehemu atakayoweza kufika ni katika Gereza la Visiwa vya Roben nchini Afrika Kusini ambako Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, kuahirishwa kwa safari ya mbugani kunatokana na gharama kubwa inayohitajika kwa ajili ya kupata walinzi maalumu wakiwemo wadunguaji wenye silaha nzito ambao watakabiliana na wanyama wakali.
Safari hii ya Obama nje ya nchi zinafanyika wakati wakala wa Serikali ikiwemo Idara Maalumu ya Ujasusi zikichuana kuhusu namna ya kupunguza matumizi.
Idara hiyo inalazimika kupunguza kiasi cha Dola 84 milioni (Sh134.2 bilioni) mwaka huu na hiyo inailazimisha kufuta safari ya kitalii ya Ikulu ya Marekani ambayo itasaidia kuokoa Dola 74,000 (Sh118.2 milioni ) kama posho ya muda wa ziada wa kazi kwa wiki kwa kila askari.
Gharama za safari hii
Safari ya sasa ya Obama itagharimu serikali kuu kati ya Dola 60 milioni hadi Dola 100 milioni (Sh 159.2 bilioni), kwa makadirio ya safari za aina hiyo zilizofanyika kwa mataifa ya Afrika miaka ya hivi karibuni.
Makadirio hayo yamefanywa na mmoja wa wataalamu wenye uzoefu na safari hizo ambaye hakutaka kutajwa jina lake kwa kuwa si msemaji rasmi.
Mwananchi

0 comments:

Post a Comment