KAMPUNI
 ya bia Tanzania (TBL)  kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager, 
inaendelea na tamasha kubwa la muziki lijulikanalo kama ‘Kili Music Tour
 2013’ wikiendi hii mjini Tanga.
Tamasha hili kubwa litafanyika Jumamosi tarehe 29 Juni, 2013 mjini Tanga kwenye kiwanja cha
 Mkwakwani na litajumuisha wasaniii 8 ambao ni Ally Kiba, Snura Mushi, 
Professor J, Mwana FA, Recho, Mzee Yusuph, Roma na Kala Jeremiah.
Tamasha
 hili ambalo hapo awali lilikuwa linajulikana kama KTMA Winners Tour 
mwaka huu lilibadilishwa jina na kuwa Kili Music Tour ili kupanua wigo 
wake na kujumuisha wasanii walioshinda tuzo za Kili Tanzania Music 
Awards, wasanii waliopendekezwa kwenye tuzo na wasanii ambao 
hawakushiriki kwenye tuzo lakini ni vinara kwenye tasnia ya muziki 
nchini.
Meneja
 wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager Bwana George Kavishe alinukuliwa 
akisema “tumeona ni jinsi gani mkoa wa Dodoma uliitikia wito na 
kushiriki kwa kikamilifu kwenye Kili Music Tour wikiendi iliyopita, 
hivyo basi tunategemea Tanga itajumuika nasi ipasavyo kufanikisha 
tamasha litakalofanyika mkoani hapo Jumamosi ya tarehe 29.”
Bwana
 Kavishe aliendelea kufafanua kuwa “mwaka huu ndani ya staili ya 
“kikwetu kwetu” bia ya Kilimanjaro Premium Lager inahakikisha kuwa kama 
kawaida inatoa bonge la kiburudisho kwa watanzania ikizingatia jinsi 
watanzania tunavyojivunia mambo yetu ya kitofauti kama muziki wetu wa 
bongo fleva, dansi yetu ya kiduku, kandanda letu lenye ushabiki wa simba
 na yanga, lugha yetu ya kipekee na bia yetu ya Kilimanjaro 
iliyotengenezwa Tanzania, kwa kutumia viungo vya kitanzania na 
watanzania.”
Msanii
 aliyebobea wa bongo flava ajulikanaye kama Professor J (Joseph Haule) 
naye alisema “wakazi wa Tanga na vitongoji vyake wasubiri shoo kubwa ya 
kufana kama waliyoipata wakazi wa Dodoma wiki iliyopita. Tunategemea 
kuwashangaza wanatanga kwa kuwapa vionjo ambayo hawajawahi kuviona kwani
 mimi na wasanii wenzangu tumejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa 
hatuwaangushi mashabiki wetu na kuwa tutawapa bonge la kiburudisho!”






0 comments:
Post a Comment