Main Menu

Wednesday, July 22, 2015

MANCHESTER UNITED YAENDELEZA UBABE MAREKANI



Depay and Rooney again showed the foundations of a good understanding as they played off each other in attackTimu ya Manchester United imeendeleza ushindi katika michezo ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu nchini England baada ya kuichapa timu ya san jose mabao 3-1 katika Uwanja wa Avaya mjini San Jose nchini marekani.

Kiungo Juan Mata ndiye alianza kuifungia United asubuhi ya leo katika dakika ya 32, kabla ya Memphis Depay kufunga la pili dakika ya 37.

San Jose walifanikiwa kupata bao lao dakika ya 42 kupitia kwa Fatai, chipukizi Andreas Pereira aliifungia man u bao la kichwa na kuihakikishia ushindi timu hiyo.
 Juan Mata (No 8) is congratulated by his team-mates after giving Manchester United the lead after 30 minutes in San Jose
Kikosi cha Louis van Gaal sasa kitamenyana na mabingwa wa Ulaya, Barcelona katika mchezo ujao wa michuano ya Kombe la Mabingwa wa Kimataifa Jumamosi nchini humo. 

Kikosi cha Manchester United kilikuwa; kipindi cha kwanza; Johnstone, Darmian, Jones, Blind, Shaw, Carrick, Schneiderlin, Young, Mata, Memphis na Rooney.

Kipindi cha pili: Johnstone, McNair, Smalling, Evans, Blackett, Lingard, Schweinsteiger, Herrera, Pereira, Januzaj na Wilson.

 Bastian Schweinsteiger played the second 45 minutes as he did in the win over Club America at the weekend

0 comments:

Post a Comment