Main Menu

Tuesday, May 19, 2015

DE GEA AIWEKA NJIA PANDA MAN U



De Gea was taken off injured during the game at Old Trafford as United fans urged him to stay at the clubKitendawili cha wapi kipa wa klabu ya Manchester United David De Gea  atacheza msimu ujao bado hakijateguliwa, kutokana na uvumi unaoenea kuwa kipa huyo ataichezea klabu ya Real Madrid msimu ujao.

Wakala wa David De Gea Jorge Mendez atafanya mazungumzo na klabu ya Manchester United wiki hii kujua hatma ya mteja wake.

Wiki iliyopita kocha wa Manchester United Louis Van Gaal alisema kuwa hatomzuia kipa huyo kujiunga na Real Madrid lakini endapo atapata ofa nzuri toka kwa miamba hiyo ya Hispania.

Hali ya De Gea katika klabu ya Manchester United imekuwa ya mashaka na mchezaji huyo amekuwa katika presha kubwa kutoka katika familia yake inayoishi nchini Hispania.

Mchezaji huyo amekuwa na mfanikio makubwa sana katika klabu ya Manchester United na kwakuutambua mchango wake, klabu ya Manchster United imempa mkataba mwingine utakaomfanya kulipwa kiasi cha euro laki mbili kwa juma.

Lakini De Gea bado anaonekana hayupo tayari kuendelea kuishi nchini England.

Kwa upande wa Real Madrid,wapo tayari kumtoa kipa wake Iker Cassilas ambaye uwezo wake umeonekana kupungua sana na kumchukua David De Gea.

Kipa wa zamani wa klabu ya Manchester United Raimond Van Der Gouw anaamini mrithi sahihi wa David De Gea katika klabu hiyo ni Victor Valdes.

0 comments:

Post a Comment