Main Menu

Tuesday, May 19, 2015

RAHEEM STERLING KUIAGA LIVERPOOL IJUMAA



Sterling is wanted by up to seven clubs including Arsenal, Chelsea and the two Manchester clubsMshamuliaji wa klabu ya Liverpool Raheem Sterling anatarajia kuondoka katika klabu ya Liverpool mwishoni mwa msimu huu.

Mchezaji huyo anatarajiwa kukutana na Mkurugenzi wake Ian Ayre na kocha wake Rodgers siku ya ijumaa, kuwaeleza kuwa anataka kuondoka katika klabu hiyo.

Hata hivyo klabu ya Liverpool haijasema lolote kwa sasa ingawa inaonekana bado wanamhitaji mchezaji huyo kinda mwenye umri wa miaka 20 na ambaye mkataba wake unaisha mwaka 2017.

Klabu kadhaa zimeonyesha nia ya kumsajili mchezaji huyo, ikiwemo klabu ya Manchester City, Arsenal  na Real Madrid.

Hata hivyo Kaptain wa Liverpool Steven Gerrard amemtaka Sterling kubakia katika timu hiyo na kusisitiza kuwa “ni vizuri kuwa katika klabu ambayo kocha ana imani na wewe”.

0 comments:

Post a Comment