Main Menu

Monday, May 18, 2015

CLOUDS MEDIA GROUP MABINGWA WAPYA WA SPORTS XTRA DAY JIJI LA MWANZA



Sports xtra day bonanza kwa jiji la mwanza lilifanyika mwaishoni mwa juma lililopita na kuwashuhudia waandaaji clouds media group wakitwaa ndoo ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwake miaka mitatu iliyopita.

Katika bonanza hilo lililofanyika katika uwanja wa ccm kirumba lilishirikisha makampuni kumi ya jijini mwanza na kuishuhudia The Dream Team ikiifumua Bank ya Nmb kwa mikwaju ya penalt 3-2 katika mchezo wa fainal.

Clouds iliiwatoa mabingwa wa mwaka jana Dar  es salaam Fastjet kwenye hatua ya nusu fainal wakati NMB wao waliwatupa nje timu ya Cocacola.
Kampuni zilizoshiriki kwenye bonanza hilo jijini mwanza ni SAUT, MEGA TRADE INVESTIMENT, NYANZA BOTLING CO LTD, SONGORO MARINE, TCC, THAQAFA teachers, NMB, TBL MWANZA na mabingwa CLOUDS MEDIA , GROUP.
 
Baada ya kumalizana na wakazi wa mwanza sasa ni zamu ya jiji la mbeya wikiendi ijayo ya tarehe 23…jipangeeeee

0 comments:

Post a Comment