Main Menu

Friday, April 17, 2015

MWAMUZI BORA VPL KULAMBA MILLION TANO



Katika kuongeza motisha kwa waamuzi na kuwashawishi kuchezesha kwa haki mwenyekiti wa baraza la michezo la taifa ameahidi sh. Million 5 kwa mwamuzi bora.

Akifunga kozi ya waamuzi vijana 35 kutoka mikoa mbalimbali nchini Dioniz Malinzi amesema yupo tayari kutoa zawadi ya  sh. Million 5 kwa muamuzi wa kati na sh. Million 2 kwa mshika kibendera bora.

Lakini malinzi ametoa masharti kwa TFF kutoa mchanganuo wa namna walivyompata mwamuzi bora na sababu za kuwa bora.

Amesema labda zawadi hiyo inaweza kuchangia waamuzi nchini kutenda haki na kuzisaidia timu zetu kushindana kikamilifu katika michuano ya kimataifa.

0 comments:

Post a Comment