Klabu ya
liverpool inayoshiriki ligi kuu ya
England imekataa ofa mpya ya paundi milioni 40 kutoka timu ya Arsenal Kutaka
kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay Luis Suarez.
Hii ni ofa
ya pili kwa klabu Arsenal kukataliwa na Liverpool kwa kipindi kisichozidi wiki
tatu kwa mchezaji huyomwenye umri wa miaka 26 ambaye alifunga magoli 30 kwenye
mechi 44 alizocheza msimu uliopita.
Haijajulikana
Liverpool inahitaji kiasi gani iliwakubali ofa ya washika bunduki hao wa jiji
la London ambao wameshikilia msimamo wa kutaka kumsajili mshambuliaji ambaye
ameifungia klabu yake magoli 51 kwenye mechi 96 za mashindano yote.
Kama Arsenal
watatuma ofa itakayozidi paundi milioni 50 huenda ikakubaliwa kutokana kauli ya
kocha wa Liverpool Brendan Rodgers
kufananisha dau la uhamisho la paundi milioni 55 wa Edinson Cavani kwenda PSG
ndio thamani halisi ya luis suarez .
0 comments:
Post a Comment