Kocha wa
klabu ya Chelsea Jose Mourinho ameipa nafasi kubwa timu ya Manchester city
kufanya vizuri na hata kuchukua taji la ligi kuu nchini England kutokana na
kufanya usajili mzuri pia wana meneja mzuri.
Wametumia
zaidi ya paundi milioni 90 kufanya usajili wa wachezaji mahiri na wazoefu wanne
pia kocha raia wa Chile Manuele Pelegrini
ambaye pia msimu uliopita alifikisha klabu ya Malaga nusu fainali ligi ya mabingwa wa ulaya.
Wachezaji hawa wataongeza ubora
kwenye kikosi cha Manchester City na kuongeza ushindani na wataleta utofauti
kati ya wao waliosajili wachezaji bora na timu ambazo hazijafanya usajili .
Manchester city imewasajili Fernandinho kutoka Shakhtar Donetsk, Jesus Navas, Alvaro
Negredo kutoka Sevilla na kiungo mshambuliaji
wakimataifa wa Montenegro Stevan Jovetic,kutoka klabu ya Fiorentina.
na issa maenda wa ebony fm
0 comments:
Post a Comment