Serikali ya Myanmar ikiwa na lengo la kuweka sheria za kibaguzi dhidi ya
Waislamu wa nchi hiyo, imepitisha sheria ya ukomo wa kuzaa watoto
wawili tu kwa Waislamu wa nchi hiyo.
Taarifa zinasema kuwa, sheria hiyo
imepitishwa na kamisheni ya familia nchini humo.
Kamisheni hiyo imeeleza
kuwa sheria ya ukomo wa kuzaa watoto wawili tu imewekewa Waislamu tu na
kwamba Mabudha wanaruhusiwa kuzaa zaidi ya idadi hiyo.
Makundi ya
kutetea haki za binadamu yamekosoa vikali sheria hiyo na kusema kuwa
inakiuka wazi haki za binadamu.
Waislamu wa Myanmar wanakabiliwa na hali
ngumu ikiwa ni pamoja na kuchomwa moto nyumba zao, kunyanyaswa,
kudhalilishwa na hata kuuawa, vitendo vinavyofanywa na Mabudda wenye
misimamo ya kufurutu mipaka.
Chanzo radio tehran
Monday, May 27, 2013
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment