Main Menu

Friday, June 19, 2015

TWFA KUFANYA UCHAGUZI AGOSTI 15



Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA), George Mushumba ametangaza uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika agosti 15, 2015 kujaza nafasi mbalimbali.

Kwa mamlaka aliyonayo ametangaza uchaguzi mkuu wa TWFA leo kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi, uchaguzi huo utafanyika tarehe 15, Agosti 2015 katika nafasi zifuatazo:

    i.        Mwenyekiti
   ii.        Katibu Msaidizi
 iii.        Mweka Hazina
iv.        Wajumbe wawili wa Kamati ya Utendaji.       

Fomu za kuomba nafasi hizo zitaanza kutolewa tarehe 19-23 Juni 2015 katika ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar es salaam.

0 comments:

Post a Comment