Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa
Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA), George Mushumba
ametangaza uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika agosti 15, 2015 kujaza
nafasi mbalimbali.
Kwa mamlaka aliyonayo ametangaza
uchaguzi mkuu wa TWFA leo kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi, uchaguzi
huo utafanyika tarehe 15, Agosti 2015 katika nafasi zifuatazo:
i.
Mwenyekiti
ii.
Katibu Msaidizi
iii.
Mweka Hazina
iv.
Wajumbe wawili wa Kamati ya
Utendaji.
Fomu za kuomba nafasi hizo zitaanza
kutolewa tarehe 19-23 Juni 2015 katika ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar
es salaam.
0 comments:
Post a Comment