Ban Ki moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameendelea na safari yake
ya kuzitembelea nchi za eneo la Maziwa Makubwa la katikati mwa Afrika
iliyoanzia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Jana Katibu Mkuu huyo wa
Umoja wa Mataifa aliwasili katika mji wenye mgogoro wa kivita wa Goma wa
mashariki mwa Kongo DRC kwa lengo la kuizindua jamii ya kimataifa
kuhusu nchi hiyo iliyokumbwa na vita vya ndani kwa miaka mingi sasa huku
mamilioni ya watu wakiendelea kuteseka kutokana na mgogoro huo.
Ban Ki
moon aliwasili mjini humo masaa machache baada ya waasi wa M23 kutangaza
kusimamisha vita karibu na mji huo ili kuruhusu kufanyika kwa usalama
safari ya Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa.
Safari fupi ya Ban
katika mji huo wenye utajiri mkubwa wa madini imefanyika siku tatu tu
tangu mapigano makali yazuke kwenye eneo hilo kati ya wanajeshi wa
serikali na waasi.
Watu wasiopungua 20 wameripotiwa kuuawa katika
mapigano hayo mapya yaliyoanza siku ya Jumatatu huku makombora
yakiripotiwa kuanguka karibu na mji huo.
Mbali na Kongo, Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa ametembelea pia nchi jirani na Kongo yaani Rwanda na
anatarajiwa kutembelea pia Uganda.
0 comments:
Post a Comment