Main Menu

Thursday, May 23, 2013

OBAMA ATETEA MATUMIZI YA NDEGE ZISIZOTUMIA RUBANI

Rais Obama ametetea sera ya matumizi ya ndege  zisizokuwa na rubani katika kile alichokiita vita halali.

Katika hotuba muhimu aliyoitoa kwenye chuo kikuu cha ulinzi wa taifa cha Washington, Obama  alisema matumizi ya ndege hizo yameifanya Marekani iwe salama zaidi. 

Hata hivyo amesisitiza kwamba inapasa kuhakikisha kuwa katika matumizi ya ndege hizo hakuna raia anaeudhurika.  

Rais Obama pia amesema utawala wake upo tayari  kukubali udhibiti zaidi wa mashambulio yanayofanywa  na ndege zisizokuwa na rubani, nje ya maeneo ya vita kama Afghanistan.

Amesema Marekani ipo vitani dhidi ya kundi ambalo  lingewaua Wamarekani wengi kwa kadri ambavyo  ingeliwezekana ,laiti hatua zisingelichukuliwa kwanza  kulizuia kundi hilo.  

Juu ya juhudi za kuifunga jela ya Guantanamo, Rais Obama alifahamisha kuwa Marekani imeiondoa hatua  ya kuusimamisha kwa muda, mpango wa kuwahamisha wafungwa na kuwapeleka Yemen. 

Katika hotuba yake kwenye chuo kikuu cha ulinzi  wa  taifa mjini Washington, Obama aliwaambia  Wamarekani kwamba jela ya Guantanamo imegeuka  kuwa ishara duniani kote, inayoonyesha jinsi Marekani inavyokiuka sheria.

0 comments:

Post a Comment