Main Menu

Sunday, January 13, 2013

WABUNGE KUANZA KAZI KATIKA KAMATI MBALIMBALI ZA BUNGE, RATIBA IPO HIVI....


Mkurugenzi  msaidizi wa Idara ya Habari Elimu kwa Umma na Ushirikiano wa Kimataifa  Deogratius  Egidio ametoa ratiba ya shughuli za kamati za bunge kabla ya kuanza kwa mkutano wa kumi wa bunge unaotarajiwa kuanza januari 29 mjini Dodoma.

Egidio  amesema mpaka sasa ofisi ya bunge haijapokea miswada yeyote badala yake kabla ya bunge kuanza wabunge kupitia kamati zao watakuwa na ziara za kutembelea maeneo mbalimbali hapa nchini.

Ametaja baadhi ya maeneo na kamati zitakazotembelea kuwa ni pamoja na kamati ya bunge ya mambo ya nje, ulinzi na usalama  na januari 15  itapokea taarifa ya hali ya ulinzi na usalama kwa kipindi cha julai hadi Desemba 2012 ambapo jumatano watapokea taarifa ya hali ya ushirikiano wa kimataifa na diplomasia duniani hadi kufikia mwezi desemba 2012.

Alhamisi kamati hiyo inatarajia kutembelea gereza la segerea ambapo ijumaa itapokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya APRM Tanzania.

Kamati nyingine ni ile ya Hesabu za serikali ambapo watajadili rasimu ya hesabu zilizokaguliwa za mafungu mbalimbali kuanzia januari 7 hadi 26 na kamati ya miundombinu  januari 15 inatarajiwa kupokea taarifa ya utendaji wa shirika la ndege Tanzania ATCL na januari 16 itapokea taarifa ya utendaji wa SUMATRA.

Amesema ratiba zote hizo zinatarajiwa kuanza saa tatu kamili katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es salaam.




 
          Bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania

0 comments:

Post a Comment