Main Menu

Friday, January 18, 2013

MKATA UPEPO KWA BAISKELI LANCE ARMSTRONG AKIRI KUTUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU

                                                    Lance armstrong

Bingwa wa zamani wa mbio za baskeli maarufu kama Tour de France, Lance Armstrong amekiri kutumia madawa za kumuongezea nguvu, katika mahojiano na mtayarishaji wa vipindi vya kijamii katika televisheni, Oprah Winfrey. 

Alipoulizwa na Oprah kama alitumia madawa ili kushinda mbio hizo, kwa mara ya kwanza Armstrong alisema ''Ndio''. 

Armstrong alikiri kuwa bila matumizi ya dawa hizo asingeweza kushinda mbio hizo mara saba. Lance Armstrong alivuliwa mataji yake yote baada ya shirika la kimarekani la kupambana na matumizi ya madawa katika michezo kutoa ripoti yake mwezi Oktoba mwaka jana.

 Armstrong alipigwa marufuku kushiriki katika michuano, na kupoteza udhamini wote kwa fuko lake la Livestrong, alilolianzisha kupambana na ugonjwa wa saratani.

dwswahili

0 comments:

Post a Comment