Main Menu

Thursday, January 17, 2013

ASKARI WA UMOJA WA SFRIKA WAWAPIGA RISASI WATOTO WATANO NCHINI SOMALIA, ETI NI BAHATI MBAYA


 
vyanzo vya habari kutoka Somalia zinaarifu kuwa, askari wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika, wamewaua kwa kuwapiga risasi raia saba wa nchi hiyo kwa bahati mbaya. 

vyanzo hivyovinaarifu kuwa, mauaji hayo yalitokea jana katika operesheni za kuwasaka wanamgambo wa ash-Shabab waliodhaniwa kwamba walikuwa wamekimbilia katika shule moja na hivyo kupelekea raia saba kuuawa wakiwamo watoto watano. 

Dhahir Amin Jisu mmoja wa wabunge wa Somalia amenukuliwa akisema kuwa, wahanga wa mauaji hayo ni watoto walio chini ya umri wa miaka 10 na kwamba tukio hilo lilitokea katika mji wa Liju ulioko umbali wa kilomita 120 kutoka mji mkuu wa Somalia, Mogadishu. 

Vikosi vya Umoja wa Afrika viko nchini Somalia kwa shabaha ya kuisaidia serikali ya nchi hiyo kupambana na wanamgambo wa ash Shabab ambao wana lengo la kuing'oa madarakani serikali ya Mogadishu kwa tuhuma kwamba, ni kibaraka wa nchi za kikafiri.

radio tehran

0 comments:

Post a Comment