Main Menu

Friday, March 14, 2014

RAIS WA TFF JAMAL MALINZI ABARIKI MKUTANO WA KATIBA SIMBA SC

Klabu ya Simba itafanya mkutano wa wanachama wake Jumapili (Machi 16 mwaka huu) kwa ajili ya kuifanyia marekebisho Katiba yao.

Nachukua fursa hii kuwatakia kila la kheri katika mkutano huo ambao ni muhimu katika kuhakikisha klabu yao inapiga hatua katika maendeleo ya mpira wa miguu na ustawi wake kwa ujumla.

Hata hivyo, nawakumbusha viongozi na wanachama wa klabu ya Simba kuwa marekebisho hayo ni lazima yafanyike kwa kuzingatia Katiba, Kanuni na maelekezo ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Afrika (CAF) na Tanzania (TFF).

Aidha waraka wa TFF kwa wanachama wake wa Februari 7 mwaka huu uzingatiwe kikamilifu katika marekebisho hayo.

TFF inawatakia wanachama wa Simba mkutano mwema, na inawakumbusha wazingatie umuhimu wa kudumisha amani na maelewano katika klabu yao.

Jamal Malinzi
Rais
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

0 comments:

Post a Comment